Wednesday 14 December 2016

Serikali Yamwaga Ajira za Walimu wa Sayansi na Hisabati


 
SERIKALI imetangaza kuajiri walimu wa masomo ya sayansi na hisabati katika shule za sekondari ambao wametakiwa kupeleka nakala za vyeti vyao vya elimu ya sekondari, vya taaluma ya ualimu (stashahada na shahada) kwa ajili ya uhakiki.

Tangazo kwa Umma lililotolewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Maimuna Tarish lilisema vyeti vya sekondari vinavyotakiwa kuhakikiwa ni vya kidato cha sita.

Alisema ajira hizo ni kwa walimu wa Stashahada na Shahada za Mafunzo ya Ualimu wa Masomo ya Hisabati na Sayansi waliohitimu mwaka 2015.

Alisema nakala hizo ziwasilishwe kupitia barua pepe ya wizara kuanzia jana hadi Ijumaa ya Desemba 16 mwaka huu na yeyote ambaye vyeti vyake havitahakikiwa hatafikiriwa katika uajiri.
Share:

MR Nice Afunguka Haya Baada ya Kuzushiwa Amefariki Dunia.....

Msanii mkongwe wa muziki, Mr Nice amesikitishwa na watu ambao wamemzushia kifo katika mtandao wa kijamii.


Mtandao mmoja wa kijamii uliandika taarifa za uongo kwamba muimbaji huyo amefariki akiwa nchini Tanzania.

Mr Nice ambaye yupo nchini Kenya amesema alishangaa kuona watu wakimpigiwa simu kwa nyingi na kuulizwa kuhusu afya yake na alivyofuatilia akagundua kuna mtandao umeandika taarifa za uongo kwamba amefariki.

Kupitia facebook, Mr Nice aliamua kuandika taarifa hii:

East africa vibes nawashukuruni sana kwa kunizushia kifo sina la kuwajibu ,,ila mungu awalipe kadri ya vile mnavyostaili kwa hiki mlichonizushia leo ….mungu ni wetu sote na hasikilizi amri za binadamu so atakaponihitaji ataniita kwa mapenzi yake but si nyie east african vibes mnaoweza kuniua wala yeyote yule chini ya hili jua …kama nyie hamuioni thamani yangu hilo ni juu yenu kwani huku niliko mimi ni kama lulu na maisha yanaendelea tena kwa kiwango cha juu kabisa ..hii si mara ya kwanza kunizushia kifo na mambo mengine ya ajabu ajabu ila all in all mi nipo na bado mtaniona sana nikiendelea kuwepo ….im total dissapointed kwakweli …mungu awape stahiki yenu ..THANKS SANA EATV 13/12/2016
Share:

Monday 12 December 2016

Miss Tanzania Diana Edward aingia fainali za Beauty With A Purpose


Miss Tanzania 2016, Diana Edward, ameingia kwenye fainali za shindano la Beauty With A Purpose ambalo ni sehemu ya mashindano mbalimbali kwenye Miss World.

Beauty With A Purpose huhusisha miradi mbalimbali ya kijamii ambayo hufanywa na washiriki wa Miss World. Diana amewasilisha documentary ya masuala ya ukeketaji kwenye jamii ya watu wa Masai.

Fainali za Miss World mwaka  huu zitafanyika December 18, nchini Marekani.

Pamoja na Diana kuonesha kufanya vizuri, tangu atawazwe kuwa Miss Tanzania mwaka huu, amekuwa akipokea maneno hasi.
“I’m not beautiful Yes,I’m not focused Yes,I’m in a vacation Yes,I’m dumb Yes,I’m not up todate Yes. Who knows tomorrow ONLY God can determine your future.Thanks for those who have been and still voting for me and supporting me no matter how much Haters are pushing me back you guys are still holding my hand and lift me up,” ameandika kwenye Instagram.

“Good News My Beauty with a Purpose Documentary for Masai Dondosha Wembe has shined again to TOP 20 waiting for the TOP position and has been said ever since there has never been such a wonderful message to the beauty pageant history of Miss World.Please Keep on voting for your Tanzania’s Best Kept Secret Princess Diana,I love myself though. One rule I was born to shade tears to fight and to become a champion,” ameongeza.
Share:

Sherehe za Maulid: Waziri Mkuu Asema Serikali itaendelea kuwatumikia Watanzania wote bila kujali dini Zao

Katika kusherekea siku ya Maulid ya kuzaliwa Mtume Muhammed (S.A.W), Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema kuwa Serikali itaendelea kuwatumikia Watanzania wote bila kujali imani zao za kidini.

Majaliwa ameyasema hayo katika sherehe za kitaifa za Maulid ambazo zimefanyika mkoani Singida na kusema kuwa kuna matukio ambayo yamekuwa yakijitokeza katika jamii na katika kuyachukulia hatua za kisheria vitendo hivyo Serikali haitakuwa ikibagua mtu kutokana na imani yake ya kidini kama jinsi inavyofanya kwa shughuli za maendeleo.

“Serikali inawashukuru sana kwa kuendelea kuunga mkono jitihada ya Serikali ya Rais Magufuli, tunaamini juhudi tunazofanya za kuweka nidhamu kwa watumishi wa umma na taasisi binafsi mtaendelea kutuunga mkono, tutaendelea kuruhusu uhuru wa kuabudu na kushirikiana na viongozi wa dini lakini tu mafundisho yanayotolewa yasikiuke sheria na kanuni za nchi,

“Serikali ipo macho kupambana na tukio lolote lenye nia ya kupoteza amani ya nchi yetu, Watanzania tushirikiane kutoa taarifa ili hatua zichukuliwe, ni vyema mtambue ninyi kama viongozi na waumini ndiyo walinzi wa nchi yetu, niwambie tu kuwa Serikali itaendelea kuwatumikia Watanzania wote bila kujali dini ya mtu wala kabila,” amesema Majaliwa.

Nae Mufti Mkuu wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeiry amesema “Jambo ambalo Waislamu tunatakiwa kuwa nayo ni kupendana, tufanye kama Mtume wetu, yeye alikuwa akijenga mshikamano, akijenga upendo akijenga umoja na kama tunataka kumfata tumwige Mtume katika kupendana, tuache majungu, fitna na tuache kila kitu kisicho na faida,

“Kwanini mnagombana Waislamu na nyie ni watu wa Mungu, Waislamu tuwe na mshikamano kama tuliokuwa nao, pia tunao undugu wa Tanzania, tupendane kama Watanzania na mwenyezi Mungu ametwambia tusibague hata kama sio Waislamu, Mungu hakatazi mtu kumtendea wema mtu mwingine kama tu hakufanyi mabaya na hayo ndiyo mafunzo ya Uislamu.”
Share:

PICHA:MTOTO ALIYEENDA KUOMBA KWENYE GARI ALIBUBUJIKWA NA MACHOZI BAADA YA KUGUNDUA ALIYEKUWA ANAMUOMBA AMEWEKEWA OXYGEN ILI KUOKOA MAISHA YAKE

Mtoto aliyeenda kuomba kwenye gari alibubujikwa na machozi baada ya kugundua aliyekuwa anamuomba amewekewa oxygen ili kuokoa maisha yake.

*** Umejifunza nini hapa?
Share:

Saturday 3 December 2016

Send off ya Diana Daison Seme ukumbi kristo mfalme



 
 
Mc Elly Ngwala Kazini
 



 
































































































 
Share:

Total Pageviews

MC ELLY NGWALA

FOR BOOKING PLEASE CALL Business No: +255 713 404 646 +255 784 297 582 +255 767 404 647 Email: mcellyngwala@yahoo.com

MC ELLY NGWALA KTK POZI

My Blog List

Powered by Blogger.