Tuesday 28 February 2017

Waziri Nape: Sikupinga vita dhidi ya biashara ya dawa za kulevya bali nilishauri busara itumike

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye ametoa ufafanuzi juu ya kauli iliyonukuliwa ikionyesha kuwa alipinga vita dhidi ya dawa za kulevya iliyoanzishwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda. Amedai kuwa hakupinga vita hiyo bali alitaka busara itumike kwa washukiwa.

Waziri Nape alitoa ufafanuzi huo katika kipindi cha dakika 45 cha ITV, alipoulizwa swali na mtangazaji wa kipindi hicho kutaka kujua kuhusu kauli yake iliyoonesha kupinga utaratibu uliotumika wa kuwakamata au kuwapata watuhumiwa wa dawa za kulevya.

“Niseme kwanza ilitokea nilikuwa na mkutano na waandishi wa habari, ukienda leo ukanitaja Nape ukaniambia baada ya siku mbili njoo kituoni, hata kama nilikuwa na madawa ya kulevya nyumbani kwangu hivi unayakutaje? 
'Kwasababu kwa vyovyote vile nitayachukua, ntayaficha, ntakuja kituoni ntaripoti utanibana ntakwambia twende nyumbani kwangu ukakague mnaenda mnakagua mnakuta hamna, si basi! 
"Kwahiyo nikawa na wasiwasi kwamba inawezekana kabisa nia ilikuwa njema lakini nilidhani pangeweza kutengenezwa utaratibu bora zaidi ya namna ya kuwapata, kwasababu hapa kuna watumiaji, kuna wauzaji na wale ambao wanaleta sasa madawa ya kulevya,” alisema Nape.

Aliendelea, “Ukishughulika na mtumiaji huyu ukadhani ndiye mhalifu wako unakosea, kwasababu huyu ni muathirika na muathirika anahitaji dawa anahitaji huduma ameshaathirika, hapa wahalifu wetu nikuanzia huyu anayemletea halafu kuna huyu anayempa yule aliyemletea, sasa ili uwapate hawa wawili lazima umtumie huyu vizuri ili akupeleke kwa hawa wawili. Lakini ukimkamata huyu ukamtia ndani sasa hawa wawili watakimbia.”

“Kwahiyo mimi nikaona kwamba tunaivuruga vita yenyewe, anayeingiza madawa ya kulevya na anayesambaza kwa maana ya kuyauza, hawa ndiyo tatizo letu. Na ndio maana nikasema hebu tutumieni busara, watu wakadhani nimepinga. 
"Tena mimi nilisema mara nyingi sana tumieni busara namna ya kuiendesha vita hii. Madhara ya kutotumia busara katika vita hii ni makubwa sana, kwasababu ukimweka huyu mtu mmoja ndani hawa wengine wataendelea kuwaathiri wengine na ndiyo maana nasema hii vita tutumieni busara. 
"Hii vita ni ya kupigana kimya kimya kwasababu wanaofanya biashara hii hawaifanyi hadharani wanafanya kwa kificho. Shughulika nao kwa kificho, hii vita hakuna mahali ambapo wameshawahi pigana hadharani, tukitajana hadharani hata wenye chuki watatajana humo humo,” alisisitiza.
Share:

Mbunge Awaomba Wananchi Wampige Mawe


Mbunge wa Korogwe Vijijini, Stephen Ngonyani maarufu Profesa Majimarefu, ametoa ruhusa kwa wakazi wa jimbo lake kumwadhibu kwa kumpiga mawe iwapo atashindwa kutekeleza ahadi alizoahidi wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa 2015.

Majimarefu aliyasema hayo wakati akizungumza kwa nyakati tofauti kwenye mikutano ya hadhara na wananchi wa Vijiji vya Kwemshai, Ngulu na Mlungui, katika ziara yake jimboni mwake.

Alisema licha ya kuwa nje ya nchi kwa matibabu, lakini baada ya afya yake kuimarika amerejea nchini akiwa tayari kutatua kero za umma.

Aidha, amewaomba wapigakura wake kuendelea kushirikiana naye huku wakimpatia muda kumwezesha kuwatatulia kero hizo.
 
“Nawashukuru kwa kuniombea pale nilipokuwa nikiugua, nilikuwa nje ya nchi kwa matibabu sala zenu zimeniwezesha kuungana nanyi leo," alisema.

Aliwaeleza wananchi wa Kijiji cha Mlungi kuwa tatizo la maji na umeme viko mbioni kutatuliwa ndani ya mwaka huu na kwamba wale wanaoeneza maneno kuwa hakutafanyika kitu wanajidanganya kwa vile mambo yanakwenda sawa.

Majimarefu alisema katika kuhakikisha wananchi wanapata maendeleo, ameamua kumkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Korogwe, Mhandisi Robert Gabriel kusimamia Mfuko wa Jimbo kusaidia miradi.

Katika hatua nyingine, Majimarefu aliwashukia mahasimu wake wa kisiasa aliodai wanatumia mbinu chafu kumchafua kuhusu afya yake tangu alipougua na kwenda kutibiwa nje.

“Kuna mahasimu wangu wa kisiasa wanapita kila kijiji kuzungumzia afya yangu kwamba nimepoteza fahamu na kukatwa mguu, siyo kweli myapuuze,”alisema.

Majimarefu alisema wananchi wapuuze uzushi huo usiokuwa na msingi kwani una lengo la kuwavunja moyo kwa manufaa yao ya kisiasa.

Hata hivyo, alisema kuwa hatavunjika moyo kwa maneno hayo na badala yake yamekuwa changamoto kwake kutekeleza ahadi zake na hafanyi hayo kwa lengo la kujipatia umaarufu kama inavyodaiwa na baadhi ya watu ila ni moja ya utekelezaji wajibu wake kwa wananchi waliomchagua.

Majimarefu aliwaeleza wananchi hao kuwa wakati wa watu kufanya fitna umekwisha na uliobaki ni ule wa kusema ukweli akiwahimiza kufanya kazi sambamba na kulinda rasilimali misitu.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Korogwe Gabriel, alisema kwamba kazi yake ni kusimamia rasilimali za umma, hivyo atahakikisha kwamba yale yote yanayoanzishwa na mbunge huyo anayalinda.
Share:

Monday 27 February 2017

Total Pageviews

MC ELLY NGWALA

FOR BOOKING PLEASE CALL Business No: +255 713 404 646 +255 784 297 582 +255 767 404 647 Email: mcellyngwala@yahoo.com

MC ELLY NGWALA KTK POZI

My Blog List

Powered by Blogger.

Blog Archive