Monday 27 March 2017

Nay wa Mitego Afunguka haya baada ya Rais Magufuli kutoa amri ya kuachiwa huru

Msanii wa muziki wa hip hop Nay wa Mitego amefunguka mengi mbele ya waandishi wa habari muda mchache baada ya kuachiwa na jeshi la polisi.
Rapa huyo alishikiliwa na jeshi hilo kwa siku mbili baada ya wimbo wake mpya ‘Wapo’ kuonekana hauna maadili.
Akiongea na waandishi wa habari baada ya kutoka kituo cha polisi alipokuwa akishiliwa, Nay ameishukuru serikali pamoja na wadau mbalimbali ambao walikuwa wanampambania.
“Nawashukuru sana watu wa media, wanasheria wangu ndugu jamaa na marafiki kwa upendo waliouonyesha kwangu. Pia naishukuru serikali kwa hichi walichokifanya, sasa hivi sina kubwa la kuongea wimbo umeruhusiwa nashukuru na nimefurahi kusikia hivyo,” alisema Nay wa Mitego.
Rapa huyo amesema kwa sasa anajipanga kufanya maandalizi ya kuandaa video kwajili ya wimbo huo.
Katika taarifa iliyotolewa mapema leo na Rais Magufuli alisema wimbo huo ni mzuri lakini aongezee changamoto nyingine zilizopo kwenye jamii.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Total Pageviews

MC ELLY NGWALA

FOR BOOKING PLEASE CALL Business No: +255 713 404 646 +255 784 297 582 +255 767 404 647 Email: mcellyngwala@yahoo.com

MC ELLY NGWALA KTK POZI

My Blog List

Powered by Blogger.

Blog Archive