Wednesday 5 April 2017

Wanaume waagizwa kutokimbia mimba

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Hamisi Kigwangalla amewaagiza wanaume wanaowapa mimba wanawake kutunza mimba hizo na kulea watoto na si kukimbia na kujitokeza baada ya mtoto kuzaliwa.
Ameyasema hayo bungeni jijini Dodoma alipo kuwa akijibu swali la Mbunge wa Chakwa, Bhangwaji Meisuria (CCM) ambaye alitaka kujua baba ataipata wapi haki ya kumwona mtoto endapo wazazi wametengana.
“Kifungu cha 26(i) kimeeleza haki za mtoto endapo wazazi watakuwa wametengana, haki hizo ni pamoja na kuendelea kupewa matunzo pamoja na elimu kama ilivyokuwa kabla ya wazazi kutengana, kuishi na mzazi mmoja wapo baada ya Mahakama kujiridhisha kuwa mzazi huyo anao uwezo wa kumlea mtoto huyo,” alifafanua.
“Ninapenda kulifahamisha Bunge kuwa zipo taratibu za kufauta endapo mzazi mmoja atakosa haki ya kumwona mtoto wake. Kwa mujibu wa taratibu mlalamikaji anaishi na mtoto ili waweze kukutanishwa na kufanyiwa unasihi ili hatimaye waweze kufikia makubaliano ya pamoja ya kumlea mtoto,” alisema Kigwangalla.
Aidha Dk Kigwangalla alisema Sheria ya Mtoto Namba 21 ya mwaka 2009 imezingatia suala zima la utoaji wa malezi, matunzo na ulinzi wa mtoto.
Na Emmy Mwaipopo
Share:

0 comments:

Post a Comment

Total Pageviews

MC ELLY NGWALA

FOR BOOKING PLEASE CALL Business No: +255 713 404 646 +255 784 297 582 +255 767 404 647 Email: mcellyngwala@yahoo.com

MC ELLY NGWALA KTK POZI

My Blog List

Powered by Blogger.

Blog Archive