Sunday 12 March 2017

KAULI YA MSEMAJI WA SIMBA BAADA YA YANGA KUTOKA SARE NA ZANACO

Baada ya Yanga kulazimishwa sare ya kufungana goli 1-1 na Zanaco FC ya Zambia kwenye mchezo wa klabu bingwa Afrika uliochezwa uwanja wa taifa Jumamosi March 11, 2017, watu wameongea mambo mengi sana, miongoni mwao ni afisa habari wa klabu ya Simba Haji Manara.
Manara ame-post ujumbe kupitia ukurasa wake wa Instagram na kuwaita Yanga wasindikizaji huku akisema watu wasubiri kupata burudani mwaka ujao kutoka kwa Simba.
“Wasindikizaji safari yao imeshaiva, ni kujipanga tu na TAZARA kwenda kukamilisha ratiba. Tungoje mwakani mnyama atatupa raha wabongo,” maneno yanayosomeka kwenye account ya Instagram ya Manara.
Simba inaweza kufuzu kucheza michuano ya kimataifa (Caf Champions League au Confederation Cup) ikiwa watashinda ubingwa wa ligi kuu Tanzania bara au ubingwa wa Azam Sports Federation Cup.
Hadi sasa Simba bado ipo kwenye nafasi nzuri ya kutwaa mataji hayo yanayosimamiwa na TFF. Inaongoza ligi kwa tofauti ya pointi mbili huku zikiwa zimesalia mechi mechi sita huku ikiwa imefuzu kucheza robo fainali ya ASFC.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Total Pageviews

MC ELLY NGWALA

FOR BOOKING PLEASE CALL Business No: +255 713 404 646 +255 784 297 582 +255 767 404 647 Email: mcellyngwala@yahoo.com

MC ELLY NGWALA KTK POZI

My Blog List

Powered by Blogger.

Blog Archive