Monday 13 March 2017

Nimepumzika nafurahi maisha ya kustaafu – Kikwete

Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Jakaya Mrisho Kikwete, amesema kwa sasa amepumzika na anafurahia maisha ya kustaafu kwake.
Alizungumza hayo mjini Dodoma katika mkutano maalum wa CCM, alipopewa nafasi ya kuzungumza, pamoja na kufurahia ustaafu wake pia alifurahia ukumbi kupewa jina lake.
Alisema huku akishangiliwa “Nimepumzika na-enjoy (nafurahia) maisha ya kustaafu.”
Sambamba na kufurahia kustaafu huko alizungumzia mabadiliko yaliyofanyika ndani ya chama hicho alisema yataongeza ufanisi katika chama hicho na kuwataka wanachama kutokuwa na hofu.
Alisema mabadiliko hayo yatasaidia chama hicho kuweza kujiendesha ikizingatiwa changamoto mojawapo ya chama hicho ni gharama kubwa za uendeshaji huku vyanzo vyake vya mapato vikiwa ni ada za uanachama na kuuza mali za chama.
“Tuna wanachama milioni nane, kama wote wangekuwa wanalipa ada tungekuwa na uhakika wa Shilingi bilioni 12 na kungekuwa hakuna cha kutuhangaisha tukiongeza na ruzuku zetu.”
“Lakini kwenye ada unakuta tunapata Shilingi milioni 500 tu, gharama za mkutano wa halmashauri kuu ya taifa ni Shilingi milioni 600, hivyo lazima rais ahangaike kusaidia,” alisema Kikwete.
By: Emmy Mwaipopo
Share:

0 comments:

Post a Comment

Total Pageviews

MC ELLY NGWALA

FOR BOOKING PLEASE CALL Business No: +255 713 404 646 +255 784 297 582 +255 767 404 647 Email: mcellyngwala@yahoo.com

MC ELLY NGWALA KTK POZI

My Blog List

Powered by Blogger.

Blog Archive